Header Ads

TAARIFA KUHUSU MAZISHI YA MZEE FRANSIS MAIGE- NGOSHA

Mix

Taarifa kuhusu mazishi ya Mzee Francis Maige ‘Ngosha’

Mwili wa mzee Francis Maige Kanyasu maarufu kama Ngosha unatarajia kuagwa June 3, 2017 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili baada ya kupatikana ndugu zake.
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya imeeleza kuwa mwili huo utaagwa majira ya saa 2:30 Asubuhi katika Hospitali hiyo na utasafirishwa hadi kijijini kwao Igokero, Misungwi Mwanza kwa ajili ya mazishi.
Mzee Francis ambaye alichora Nembo ya Taifa alifariki Usiku wa May 29, 2017 akiwa kwenye matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili akiwa na umri wa miaka 86.

No comments:

Powered by Blogger.