Header Ads

Ripoti ya Prof. Osoro yaichanganya ACACIA, yaipinga huku ikitangaza kupunguza wafanyakazi 400

MuroTv

KITAIFA

Ripoti ya Prof. Osoro yaichanganya ACACIA, yaipinga huku ikitangaza kupunguza wafanyakazi 400

n
Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Acacia imetangaza kuwa na mpango wa kupunguza wafanyakazi wake wapatao 400 hasa walinzi wa mgodi huo.
Afisa Habari na Mahusiano ya Jamii wa Kampuni hiyo, Nectar Foya amesema kampuni hiyo inatarajia kuingia mkataba na kampuni binafsi ambayo itaendesha shughuli za ulinzi wa migodi yake, ikiwemo wa Bulyanhulu na Buzwagi.
“Tumeamua kuingia mkataba na kampuni ya ulinzi kwa sababu ndio njia pekee ya kulinda rasilimali zetu na kuzuia kuendelea kupata hasara,” amesema.
Katika hatua nyingine, kampuni hiyo kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa Juni 12, 2017, inapinga ripoti ya Kamati ya Pili ya Uchunguzi wa Makinikia aliyokabidhiwa Rais John Magufuli mapema hii leo na Mwenyekiti wa kamati hiyo Prof. Nehemiah Osoro Ikulu jijini Dar es Salaam. 
Taarifa hiyo ya Acacia inadai kuwa, matokeo ya uchunguzi wa kamati hiyo juu yake si ya kweli na kwamba hayaendani na uhalisia wa utendaji kazi wake hapa nchini kwa zaidi ya miaka ishirini.
FOLLOW NA LIKE PAGE YANGU YA FACEBOOK HAPA CHINI
 CLICK HAPA OPEN
FOLLOW ACCOUNT YANGU YA INSTAGRAM 
CLICK HAPA ➼ OPEN

MuroTV na murotv.blogspot.com zipo kwaajili ya kukuhabarisha kwa wakati.
Image may contain: text       KWA MATANGAZO WASILIANA NAMI KUPITIA;

Phone: 0768786851
Email:prospermuro690@gmail.com
          : prosperalphonce35@gmail.com
Instagram: muro_tv
 

No comments:

Powered by Blogger.