Header Ads

Waziri Ndalichako akabidhi zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri kitaifa

MuroTV

MATUKIO

Waziri Ndalichako akabidhi zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri kitaifa

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amewataka wanafunzi nchini kuwa na Nidhamu kwani bila nidhamu hakuna mafanikio yanayoweza kupatikana.
 
Waziri Ndalichako ametoa kauli hiyo hii leo mjini Dodoma wakati akikabidhi tuzo na zawadi mbalibali kwa  wanafunzi waliofanya vizuri katika mitihani ya kumaliza shule ya msingi, kidato cha Nne na wale wa kidato cha sita ambapo amewasisitiza wanafunzi wa kike  kujiepusheni na mapenzi wakati wakiwa mashuleni.
 
Waziri Ndalichako amewataka wanafunzi kuhakikisha wanasoma kwa bidii, ambapo pia  amewaonya wanaowanyemelea wanafunzi kwa lengo la kuwaharibia masomo na ndoto walizonazo  kuwa  sheria ni kali na  ikithibitika  muhusika atakwenda jela miaka 30.
 
 Viongozi wengine walioambata na waziri katika shughuli hiyo ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo na Naibu Katibu Mkuu Profesa Saimon Msanjila.
 
Kauli mbiu ya siku ya Elimu ni: Elimu ni nguzo muhimu kwa Maendeleo ya viwanda
 
Pia usisahau ku like page yangu ya facebook hapo chini ama kwa kunifuata Facebook Tafuta / search @ Muro Tv


FOLLOW NA LIKE PAGE YANGU YA FACEBOOK HAPA CHINI
 CLICK HAPA OPEN
FOLLOW ACCOUNT YANGU YA INSTAGRAM 
CLICK HAPA ➼ OPEN

MuroTV na murotv.blogspot.com zipo kwaajili ya kukuhabarisha kwa wakati.
Image may contain: text       KWA MATANGAZO WASILIANA NAMI KUPITIA;

Phone: 0768786851
Email:prospermuro690@gmail.com
          : prosperalphonce35@gmail.com
Instagram: muro_tv

No comments:

Powered by Blogger.