UPEPO MKALI WA KUSI KUIKUMBA PWANI YA TANZANIA
MuroTv
Upepo mkali wa Kusi kuikumba pwani ya Tanzania
Pwani ya Tanzania
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya kuwepo kwa upepo huo mkali na mawimbi makubwa katika maeneo ya pwani ya Tanzania. Mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Dar es Salaam, Tanga kwa upande wa Tanzania Bara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba kwa upande wa Zanzibar itakumbwa zaidi na upepo huo.
"Msukumo wa upepo wa Kusi unatokana na kuimarika kwa mgandamizo mkubwa wa hewa katika ukanda wa pwani ya Tanzania," ilisema taarifa ya TMA. Tahadhari kubnwa imetolewa kwa wavuvi na watumiaji wengine wa bahari hasa maeneo yaliyotajwa ili kuepuka ajali ambazo zinaweza kuepukika.
Hali hiyo ya hewa inatarajiwa kuwepo hadi kufikia kesho 31 Mei,2017.

No comments:
Post a Comment