Header Ads

Vitu saba vya kifahari unavyoweza kumiliki kwa dau alilonunuliwa nalo Neymar

 
Neymar
Baada ya Neymar kukamilisha usajili wa rekodi ya dunia wa kati ya pound milioni 199 hadi 200 akitokea FC Barcelona na kujiunga na Paris Saint Germain ya Ufaransa, kiasi ambacho kimeweka rekodi ya dunia ya uhamisho na inatarajiwa kuwa rekodi hiyo itadumu.
BBC Sport wamefanya utafiti wa vitu vya kifahari ambavyo unaweza kumiliki ukipewa pound milioni 200 ambazo ni zaidi ya Tsh Bilioni 580, kiasi hicho cha usajili unaweza ukasajili wachezaji wawili wenye thamani ya Paul Pogba.
\
Vitu 12 unavyoweza kumiliki ukipewa pound milioni 200 alizosajiliwa Neymar
1- Visiwa binafsi vinne vya Bahamas ambavyo thamani yake ni pound milioni 187.5
2- Unaweza kununua ndege binafsi 12 (Private Jets) kwa pound 188.7
Private Jets
3- Unaweza kumiliki nyumba 845 UK kwa pound milioni 200

4- Pound milioni 200 kama utaamua kukaa hoteli utaishi kwa miaka 10,000
5-Pound milioni 183 unaweza kulipia tiketi za misimu mitatu kwa siti zote za uwanja wa FC Barcelona uwanja wa Nou Camp unachukua mashabiki 99,000.
6- Unaweza kumnunulia chakula kila raia wa Chile kwa pound milioni 176
7- Unaweza kusajili mchezaji mmoja au wawili wenye majina makubwa hapa duniani

No comments:

Powered by Blogger.