Header Ads

Thomas Ulimwengu amefanyiwa upasuaji

 
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayecheza soka la kulipwa katika club ya AFC Eskilstuna ya Sweden Thomas Ulimwengu amefanyiwa upasuaji wa goti.
Thomas Ulimwengu ambaye amekuwa hafanyi vizuri wakati huu kutokana na kusumbuliwa na goti kiasi cha kuhatarisha uwezo wake uwanjani, amefanyiwa upasuaji tayari na kesho anaanza mazoezi ya kutembea.

Ulimwengu kupitia instagram account yake amethibitisha kufanyiwa upasuaji “Nashukuru Mungu oparation ya Goti imeenda poa na nimeshapata ruhusa tayar…kesho tunaanza mazoez ya mguu chini ya uangalizi wa doct… THANKS GOD.

No comments:

Powered by Blogger.