Header Ads

“Naomba tuheshimiane” Pochettino achoshwa na kelele za Conte na Mourinho

 
Kwa nyakati tofauti makocha wa Chelsea na Manchester United wamekuwa wakiizungumzia Tottenham Hotspur na wachezaji wao suala ambalo linaonekana kumkera sana kocha wa Tottenham Mauricio Pochettino.
Pochettino hapendezwi na suala la makocha hao kupenda kuizungumzia timu yake mara kwa mara huku wao Tottenham hawajawahi kuzizungumzia timu hizo.
Conte amesema wiki hii anatamani kumnunua Kane na kueleza matarajio ya Tottenham Hostpur huku Mourinho akisema Tottenham wana wakati mzuri sana kwani wamemuuza Kyle Walker tu hadi sasa tofauti na matarajio ya wengi.
“Mimi ni kocha ambaye sipendi hata kidogo kuzungumzia timu za wenzangu wala makocha wenzangu hiyo inatokana na kwa sababu nina heshima na naomba hata hao wenzangu waheshimu tunachofanya” alisema Pochettino.
Pochettino anaamini timu nyingine zina presha kubwa kwa sasa “wametumia pesa nyingi katika usajili ni lazima wako katika presha kubwa sana tofauti na sisi, sisi tuko vile vile vya siku zote hatuna cha kupoteza” aliongezea Pochettino.
Pochettino pia amesisitiza Eric Dier hataenda popote. Tottenham wamekuwa wakiwapa presha kubwa sana vigogo wa EPL katika siku za karibuni hali inayopelekea wao kutazamwa kama tatizo kwa vilabu vinavyotaka ubingwa.

No comments:

Powered by Blogger.