Header Ads

Watanzania waaswa kujitokeza kuchangia damu ilikuoa Wamama Wajawazito

MuroTV

KITAIFA

Watanzania waaswa kujitokeza kuchangia damu ilikuoa Wamama Wajawazito

Watanzania wameaswa kujitokeza kuchangia damu mara kwa mara ili kuondokana na tatizo la vifo vinavyotokana na upungufu wa damu hasa kwa kina mama wajawazito nchini wanaopoteza damu nyingi wakati wa kujifungua.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipotembelea katika tukio la uchangiaji damu lililofanyika Makao makuu ya benki ya KCB jijini Dar es salaam.
“Marufuku kwa mtoa huduma yeyote wa afya kuuza damu mgonjwa kwani  wananchi wanachangia damu bure kwa manufaa yao ya baadae aidha kwa wao wenyewe au ndugu zao” alisema Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy amewaagiza Waganga Wafawidhi wa mikoa kuhakikisha wanaweka mabango yanayoonyesha kuwa damu ni bure kwa wagonjwa wote wanaohitaji huduma hiyo bila ya kubagua mwananchi yeyote.
Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa mwananchi yeyote mwenye umri wa miaka 18, mwanamke asiye mjamzito wala  kunyonyesha na asiyekua mgonjwa kama vile kisukari,saratani na mgonjwa wa moyo  anaweza kuchangia damu.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya KCB nchini Bw. Cosmas Kimario amesema kuwa wameamua kuaandaa uchangiaji wa damu ili kuisadia Serikali katika sekta ya Afya hususani katika kupunguza vifo vinavyotokana na upungufu wa damu
 KCB wameamua kufanya hivyo ili kuelekea kuadhimisha siku ya kuchangia damu duniani ambayo hufanyika June 14 kila mwaka na maadhimisho ya mwaka huu yamebeba kauli mbiu isemayo “CHANGIA DAMU,  CHANGIA SASA CHANGIA MARA KWA MARA”.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu  katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa KCB Bank wakiwakilishwa na Mkurugenzi mtendaji wao Cosmas Kimario (Wakwanza kushoto kwa Mh.Waziri) na wadau wa Afya wakati alipotembelea katika tukio la uchangiaji damu lililofanyika Makao makuu ya benki ya KCB jijini Dar es salaam.

Mfanyakazi wa KCB Bank akijitolea damu, katika siku ya Uchangiaji damu lililofanyika katika Makao makuu ya benki ya KCB jijini Dar es salaam.

Mfanyakazi wa KCB Bank akijitolea damu, katika siku ya Uchangiaji damu lililofanyika katika Makao makuu ya benki ya KCB jijini Dar es salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na waandishi wa habari juu ya umuhimu wa kuchangia damu kwa watu wote wakati alipotembelea katika tukio la uchangiaji damu lililofanyika Makao makuu ya benki ya KCB jijini Dar es salaam.
FOLLOW NA LIKE PAGE YANGU YA FACEBOOK HAPA CHINI
 CLICK HAPA OPEN
FOLLOW ACCOUNT YANGU YA INSTAGRAM 
CLICK HAPA ➼ OPEN

MuroTV na murotv.blogspot.com zipo kwaajili ya kukuhabarisha kwa wakati.
Image may contain: text       KWA MATANGAZO WASILIANA NAMI KUPITIA;

Phone: 0768786851
Email:prospermuro690@gmail.com
          : prosperalphonce35@gmail.com
Instagram: muro_tv
   

No comments:

Powered by Blogger.