Header Ads

MAHAKAMA TAIWAN YAIDHINISHA NDOA YA WAPENZI WA JINSIA MOJA

DUNIANI

Mahakama Taiwan yaidhinisha ndoa ya wapenzi wa jinsia moja

 Mai 25,2017 Mjadala mkali kuhusu kuhalalisha ndoa za wapenzi wa jinsia moja umeigawa Taiwan

Majaji wakuu nchini Taiwan wameidhinisha ndoa za jinsia moja na kuifanya Taiwan kuwa nchi ya kwanza barani Asia kuhalalisha ndoa za mapenzi ya jinsia moja.
Mahakama kuu imesema sheria za sasa za kuwazuia watu wa mapenzi ya jinsia moja kuoana zinakiuka haki yao ya usawa na ni kinyume cha Katiba.
Mahakama hiyo imelipa bunge la nchi hiyo miaka miwili kufanyia mabadiliko ya sheria za sasa au lipitishe sheria mpya.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Mahakama imesema kutowaruhusu watu wawili wa jinsia moja kuoana kwa madai ya kulinda maadili ni sawa na "ubaguzi" "bila kufuata msingi wowote"

No comments:

Powered by Blogger.