Header Ads

Okwi amewasili Dar es Salaam kimya kimya kujiunga na Simba


Baada ya mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba SC Zacharia Hans Pope kuthibitisha kuwa mshambuliaji wao wa zamani wa kimataifa wa Uganda Emanuel Okwi ataingia Dar es Salaam Jumamosi ya June 24, usiku wa June 24 ni kweli ameingia Dar es Salaam.

Kaburu tayari kwa kuondoka Airport baada ya kumpokea Okwi.
Licha ya kuwa Hans Pope alitaja siku lakini muda na ndege anayokuja nayo ilifichwa kwa lengo la kuepuka waandishi wa habari wasimpate.
Kwa taarifa za awali mshambuliaji huyo aliyewahi kuichezea Simba kwa nyakati mbili tofauti, atajiunga na Simba kwa mkataba wa miaka miwili kabla ya kurudi kwao Uganda akisubiri maandalizi ya msimu mpya wa Ligi.

No comments:

Powered by Blogger.