Header Ads

Mwenyekiti Uvccm wilayani Arusha awapongeza wawekezaji kwa uzalendo wanaonyesha

Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Arusha mjini amewapongeza wawekezaji wazalendo wanaosaidia maendeleo ya wananchi wanaowazunguka Mwenyekiti huyo ameyasema hayo leo Kata ya Themi alipomtembelea mwenyekiti wa mtaa wa Kambarage  Ancleus Karata ambaye pia ni mjumbe wa baraza kuu wilaya ya Arusha mjini 
 
Mwenyekiti karata amemtembeza  Mh: Munisi kwenye miradi mbali mbali ya mendeleo ambayo ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM mradi wa maji ambao umefadhiliwa na SUN FLAG umemaliza tatizo la maji kwa 96%
Pia vivuko ambavyo vimejengwa kwa nguvu za wananchi na kimoja kikubwa kinachounganisha kata ya Engutoto na Themi kilichofadhiliwa na wawekezaji SOLNIL ARUSHA SUNDRIERS pamoja na HANS PAUL
 
Mh Munisi akizungumza kwenye ziara hiyo alisema   
 
" Nawaonya, Chadema waache kutembea kwenye miradi ambayo siyo ilani yao wao walishindwa vibaya uchaguzi mkuu 2015 wenyehaki yakutembelea na kuhoji juu ya miradi ya maendeleo ni CCM maana sisi ndiyo wananchi waliingia mkataba na sisi 2015 -2020 na uchaguzi ujao watakuja kutuuliza sisi CCM na siyo chadema "
 
 " Hata hivyo ninawapongeza  sana wilaya ya Ubungo kwa kuwazuia Chadema kwenda kwenye miradi wao wasubirie siku wakijaga kushinda miaka mia ijayo ndiyo waje kukagua siyo sasa kwasasa ni sisi ccm"

No comments:

Powered by Blogger.