Header Ads

Boko Haram washambulia tena Nigeria

MuroTV

Boko Haram washambulia tena Nigeria

  7 June 2017Wapiganaji wa Boko HaramWapiganaji wa Boko Haram

Wapiganaji wa Boko Haram wamefanya mashambilizi makali katika mji ulioko kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Watu walioshuhudia wanasema mashambulizi hayo makali yametokea wakati waislamu wakijiandaa kufuturu katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Picha ya video ambayo haijathibitishwa iliyotumwa katika mtandao wa Twitter inaonesha wanawake na watoto wakikimbia kutokana na mashambulizi hayo.
Gavana wa mji huo Kashim Shettima amesema kwamba kulikuwa na majeruhi.
Lakini hata hivyo amesema jeshi la nchi hiyo limejibu mashambulizi na mji tayari ni shwari.
Wapiganaji wa Boko Haram wameteketeza eneo la kaskazini mashariki mwa Nigeria kwa kuua maelfu ya watu na kulazimisha wengine milioni mbili kuyakimbia makazi yao.

MuroTV na murotv.blogspot.com zipo kwaajili ya kukuhabarisha kwa wakati.
Image may contain: text KWA MATANGAZO WASILIANA NAMI KUPITIA; 
Phone: 0768786851
Email:prospermuro690@gmail.com
          : prosperalphonce35@gmail.com
Instagram: muro_tv

No comments:

Powered by Blogger.