SAMSUNG WAJA NA PROMOSHENI YA NUNUA SAJILI NA USHINDE
MuroTV
MATUKIO
SAMSUNG WAJA NA PROMOSHENI YA NUNUA SAJILI NA USHINDE
Bi Lailatu Jethwa Meneja
Mauzo Samsung (Kushoto) akiwaonyesha waandishi wa habari stika mbili
zinazolenga kutokomeza bidhaa feki nchini katika mkutano na waandishi wa
habari uliofanyika jijini Dar es Salaam Jana. Katikati ni, Meneja wa
Samsung Nchini Bw Rayton Kwembe, akifatiwa na meneja bidhaa wa Samsung
Bw Elias Mushi, Meneja wa Phyramid consumers Karen Babu na Lulu Chiza
Mkurugenzi wa masoko Phyramid consumers.
Bi Lailatu Jethwa Meneja
Mauzo Samsung (Kushoto) akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na
kampeni yao mpya ya Nunua sajili na Ushinde inayolenga kutokomeza bidhaa
feki nchini katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini
Dar es Salaam Jana. Katikati ni, Meneja wa Samsung Nchini Bw Rayton
Kwembe, akifatiwa na meneja bidhaa wa Samsung Bw Elias Mushi na Meneja
wa Phyramid consumers Karen Babu
Bi Lailatu Jethwa Meneja
Mauzo Samsung (Kushoto) akiwaonyesha waandishi wa habari bidhaa
zinazohusishwa katika kampeni yao mpya ya ‘Nunua sajili na Ushinde’
inayolenga kutokomeza bidhaa feki nchini katika mkutano na waandishi wa
habari uliofanyika jijini Dar es Salaam Jana. Kulia ni, Meneja wa
Samsung Nchini Bw Rayton Kwembe.
…………………………..
Samsung wazindua stika mbili za kupambana na bidhaa feki
Samsung wazindua stika mbili kwa utambuzi wa bidhaa Halisi
Samsung waungana na Pyramid consumers kukuza soko Tanzania
Dar es salaam, June
2017. Samsung Tanzania wameanzisha mfumo wa kuweka stika mbili katika
bidhaa zao kwa ajili ya utambuzi wa bidhaa zao halisi pamoja na
kupambana na bidhaa feki nchini. Sambamba na mkakati huo Samsung
piawameanzisha Kampeni ya ‘Nunua Sajili na Ushinde’. Kampenihiyo ya
mwezi mzima inayolenga kutokomeza bidhaa feki nchini itaanza tarehe 16
ya mwezi juni katika mikoa yote ya Tanzania, na itaambatana na
promosheni kabambe inayotarajiwa kuwazawadia mamilioni ya watanzania
watakao nunua bidhaa halisi za Samsungkama vile TV, Friji, Microwave,
mashine ya kufulia pamoja na Viyoyozi.
“Ukizingatia bidhaa
feki zina hatarisha afya za watumiaji, mahitaji ya bidhaa bora na halisi
yanaongezeka kwa kasi kila kukicha. Samsung tumeendelea kufanya
jitihada zaidi katika kukidhi matakwa ya wateja wetu ulimwenguni pamoja
na Tanzania kwa ujumla. Samsung Tanzania inaamini kwamba kampeni ya
‘Nunua, Sajili, Na Ushinde’ itaongeza uzoefu mpya na uelewa kwa wateja
wetu wa dar es salaam na mikoani pia juu ya utambuzi wa bidhaa feki
zisizo kuwa za Samsung” alisema Meneja Bidhaa kutoka Samsung, Bw. Elias
Mushi.
Akiongeleakuhusumkakati
huo mpya Bw Mushi alisema ‘tumeongeza alama mpya kwenye bidhaa zetu
ambazo ni stika mbili zitakazo wasaidia wateja kutambua bidhaa feki
sokoni, Bidhaa za Samsung zitakuwa na stika mbili, stika msambazaji na
stika inayotambulisha bidhaa halisi ya Samsung. Kampeni ya ‘Nunua Sajili
na Ushinde’ itakua ni kiunganishi cha kupeleka elimu kwa wateja wetu
ambayo itawapa taarifa za bidhaa zetu zinazoenda sambamba na mahitaji ya
matumizi yao.
MuroTV na murotv.blogspot.com zipo kwaajili ya kukuhabarisha kwa wakati.
KWA MATANGAZO WASILIANA NAMI KUPITIA;
Phone: 0768786851
Email:prospermuro690@gmail.com
: prosperalphonce35@gmail.com
Instagram: muro_tv
MuroTV na murotv.blogspot.com zipo kwaajili ya kukuhabarisha kwa wakati.
KWA MATANGAZO WASILIANA NAMI KUPITIA;
Phone: 0768786851
Email:prospermuro690@gmail.com
: prosperalphonce35@gmail.com
Instagram: muro_tv

No comments:
Post a Comment