Header Ads

SAMSUNG WAJA NA PROMOSHENI YA NUNUA SAJILI NA USHINDE

MuroTV

MATUKIO

SAMSUNG WAJA NA PROMOSHENI YA NUNUA SAJILI NA USHINDE


unnamed
Bi Lailatu Jethwa Meneja Mauzo Samsung (Kushoto) akiwaonyesha  waandishi wa habari stika mbili zinazolenga kutokomeza bidhaa feki nchini katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam Jana. Katikati  ni, Meneja wa Samsung Nchini Bw Rayton Kwembe,  akifatiwa na meneja bidhaa wa Samsung Bw Elias Mushi, Meneja wa Phyramid consumers Karen Babu na Lulu Chiza Mkurugenzi wa masoko Phyramid consumers.

1

Bi Lailatu Jethwa Meneja Mauzo Samsung (Kushoto) akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na kampeni yao mpya ya Nunua sajili na Ushinde inayolenga kutokomeza bidhaa feki nchini katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam Jana. Katikati  ni, Meneja wa Samsung Nchini Bw Rayton Kwembe,  akifatiwa na meneja bidhaa wa Samsung Bw Elias Mushi na Meneja wa Phyramid consumers Karen Babu

2

Bi Lailatu Jethwa Meneja Mauzo Samsung (Kushoto) akiwaonyesha  waandishi wa habari bidhaa zinazohusishwa katika kampeni yao mpya ya ‘Nunua sajili na Ushinde’ inayolenga kutokomeza bidhaa feki nchini katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam Jana. Kulia  ni, Meneja wa Samsung Nchini Bw Rayton Kwembe.

…………………………..

Samsung wazindua stika mbili za kupambana na bidhaa feki

Samsung wazindua stika mbili kwa utambuzi wa bidhaa Halisi

Samsung waungana na Pyramid consumers kukuza soko Tanzania

Dar es salaam, June 2017. Samsung Tanzania wameanzisha mfumo wa kuweka stika mbili katika bidhaa zao kwa ajili ya utambuzi wa bidhaa zao halisi pamoja na kupambana na bidhaa feki nchini. Sambamba na mkakati huo Samsung piawameanzisha Kampeni ya ‘Nunua Sajili na Ushinde’. Kampenihiyo ya mwezi mzima inayolenga kutokomeza bidhaa feki nchini itaanza tarehe 16 ya mwezi juni katika  mikoa yote ya Tanzania, na itaambatana na promosheni kabambe inayotarajiwa  kuwazawadia mamilioni ya watanzania  watakao nunua bidhaa halisi za Samsungkama vile TV, Friji, Microwave, mashine ya kufulia pamoja na Viyoyozi.

 “Ukizingatia bidhaa feki zina hatarisha afya za watumiaji, mahitaji ya bidhaa bora na halisi yanaongezeka kwa kasi kila kukicha. Samsung tumeendelea kufanya jitihada zaidi katika kukidhi matakwa ya  wateja wetu ulimwenguni pamoja na Tanzania kwa ujumla. Samsung Tanzania inaamini kwamba kampeni ya ‘Nunua, Sajili, Na Ushinde’ itaongeza uzoefu mpya na uelewa  kwa wateja wetu wa dar es salaam na mikoani pia juu ya utambuzi wa bidhaa feki zisizo kuwa za Samsung” alisema Meneja Bidhaa kutoka Samsung, Bw. Elias Mushi.

Akiongeleakuhusumkakati huo mpya Bw Mushi alisema ‘tumeongeza alama mpya kwenye bidhaa zetu ambazo ni stika mbili zitakazo wasaidia wateja kutambua bidhaa feki sokoni, Bidhaa za Samsung zitakuwa na stika mbili, stika msambazaji na stika inayotambulisha bidhaa halisi ya Samsung. Kampeni ya ‘Nunua Sajili na Ushinde’ itakua ni kiunganishi cha kupeleka elimu kwa wateja wetu ambayo itawapa taarifa za bidhaa zetu zinazoenda sambamba na mahitaji ya matumizi yao.
MuroTV na murotv.blogspot.com zipo kwaajili ya kukuhabarisha kwa wakati.
KWA MATANGAZO WASILIANA NAMI KUPITIA;
Phone: 0768786851
Email:prospermuro690@gmail.com
           : prosperalphonce35@gmail.com 
Instagram: muro_tv
 

No comments:

Powered by Blogger.