Header Ads

ZANZIBAR YADHIBITI UCHIMBAJI MCHANGA

MuroTv

Zanzibar yadhibiti uchimbaji mchanga 

 31 Mai 2017

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud Mohamed
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeamua kuratibu uchotaji wa mchanga kulinda uharibifu wa mazingira uliopo sasa unaotishia kutoweka kwa rasilimali hiyo. Hayo yalisemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud Mohamed wakati akitoa ufafanuzi wa kauli ya Serikali kuhusu suala hilo.
Mohamed alitoa ufafanuzi huo baada ya baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kupinga hatua ya Serikali kuratibu kazi za uchotaji wa mchanga katika machimbo ya mkoa wa Kaskazini Unguja.
Alisema Serikali haina nia ya kupora mali ya mtu lakini kilichofanyika ni kudhibiti na kusimamia uchotaji huo wa mchanga baada ya kutokea kwa athari mbalimbali. Kwa mfano alisema katika kipindi ambacho wananchi walikuwa wakiratibu wenyewe, athari kubwa za kimazingira zilijitokeza.
Alizitaja athari hizo kuwa ni baadhi ya maeneo yaliyochotwa mchanga kutofaa tena kwa kilimo ambapo wakulima wengi wanalalamikia kukosa chakula cha kutosha. Alisema maeneo hayo hayafai kwa kilimo kwa sababu mchanga umechotwa bila maelekezo ya kitaalamu ikiwemo kwenda chini zaidi na hivyo kuondoa rutuba ardhini.
Alisema athari za kimazingira zimechangia maji chumvi kuingia katika mabonde hayo na kusababisha mmomonyoko wa ardhi. Alisema athari hizo ndizo zilizosababisha Serikali kuchukua jukumu la kuratibu kazi za uchotaji wa mchanga na si kufanya biashara. Zanzibar ina uhaba mkubwa wa mchanga kiasi cha kuweka utaratibu mzuri wa udhibiti wake ikiwemo kuendesha biashara hiyo.

No comments:

Powered by Blogger.