Header Ads

BREAKING: Wallece Karia ashinda urais TFF, Michael Wambura kuwa Makamu wake

Rais mpya wa Shirikisho la soka nchini (TFF), Walles Karia

Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini TFF umehitimishwa kwa aliyekuwa makamu wa Rais wa Shirikisho hilo Wallace Karia kushinda kwa jumla ya kura 95 na kuwabwaga wapinzani wake.


Uchaguzi huo umefanyika leo mkoani Dodoma ukiwa wa amani kwa wajumbe wa mkutano mkuu pamoja na wagombea wenyewe.


Mwenyekiti wa kamati ya Uchaguzi wa TFF, Wakili Revocatus Kuuli akitangaza matokeo hayo ambapo alimtangaza Walace Karia kama mshindi wa kinyang'anyiro kwa kura 95 kati ya kura 127, akifuatiwa na Ally Mayay mwenye kura 9 sambamba na Shija Richard.


Kuuli ametangaza kuwa, katika nafasi ya makamu wa Rais, Michael Richard Wambura ameweza kushinda katika nafasi hiyo kwa kura 85.


Kwa upande wa wajumbe wa mkutano mkuu kumekuwa na maingizo mapya kutoka kanda mbalimbali za nchini.


Zone 1: Saloum Chama 

Zone 2: Vedastus Lufano 

Zone 3: Mbasha Matutu 

Zone 4: Sarah Chao 

Zone 5: Issa Bukuku 

Zone 6: Kenneth Pesambili 

Zone 7: Elias Mwanjala 

Zone 8: James Mhagama 

Zone 9: Dunstan Mkundi 

Zone 10: Mohamed Aden 

Zone 11: Francis Ndulane 

Zone 12: Khalid Abdallah 

Zone 13: Lameck Nyambaya
Makamu wa Rais mpya wa Shirikisho la soka nchini (TFF), Michael Wambura .






http://murotv.blogspot.com/

No comments:

Powered by Blogger.