Header Ads

WAKILI AELEZA SHERIA KUHUSU KUFUKULIWA KABURI LA IVAN

MuroTv

Wakili aeleza sheria kuhusu kufukuliwa Kaburi la Ivan

June 2, 2017 Mahakama Kuu Uganda iliomba kufukuliwa Kaburi la aliyekuwa Mfanyabiashara maarufu Uganda Ivan Ssemwanga na kutolewa fedha zilizotupwa hatua iliyokuja baada ya Bank Kuu kutoa tamko kuvitaka Vyombo vya Dola kuwachukulia hatua waliotupa fedha hizo…sheria inasemaje?
Kufuatia ombi hilo la Mahakama ya Uganda leo June 3, 2017. Wakili wa kujitegemea na Mwanaharakati wa Haki za Binadamu Tanzania Jebra Kambole ambaye anafafanua zaidi…
“Nilichokiona kwenye shauri ambalo limefunguliwa Uganda ni maombi ambayo yamefikishwa Mahakamani na Mahakama ndiyo ina jukumu la kuyatafsiri yale maombi. Kwa hiyo siyo amri ya Mahakama moja kwa moja.
“Ni maombi ambayo yamepelekwa chini ya kifungu namba 42, kifungu pia cha 17, kifungu kidogo cha kwanza (a) na (i) ya Katiba ya Uganda ya mwaka 1965, lakini pia kifungu cha 50 cha Katiba ya Uganda.
“Kimsingi, vifungu hivyo ambavyo nimevitaja hapo awali vya Katiba ya Uganda ni vifungu ambavyo moja kwa moja vinatoa wajibu kwa kila raia kuheshimu alama za Taifa ikiwemo pamoja na pesa ya nchi.” – Jebra Kambole.
 SIKILIZA NYIMBO MPYA YA KING DAVY-KWA MUDA

No comments:

Powered by Blogger.