Header Ads

Serikali Imetangaza rasmi, nafasi za kazi 15,000 katika sekta mbali mbali za Umma.

MuroTV

AJIRA MPYA

Serikali Imetangaza rasmi, nafasi za kazi 15,000 katika sekta mbali mbali za Umma.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki amesema tayari serikali imetoa kibali cha ajira 15,000 kwa ajili ya kujaza nafasi zilizoachwa wazi na watumishi waliofutwa kazi baada ya waliobainika kuwa na vyeti vya kughushi katika kada mbalimbali.
Waziri Kairuki ameyasema hayo leo bungeni alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa, Ritta Kabati aliyetaka kujua mpango wa serikali kuhusu kujaza nafasi zilizoachwa wazi na watumishi wa umma walioacha kazi kufuatia agizo la Rais Magufuli alilolitoa mapema Mei mwaka huu.
Waziri Kairuki alisema kuwa ni kweli baada ya watumishi hao kuondoka katika vituo vyao vya kazi, sehemu mbalimbali zilikumbwa na uhaba wa watumishi na hivyo kupelekea kuzorota kwa utoaji wa huduma. Lakini ili kukabailiana na hilo, hivi karibuni serikali imetoa kibali cha kuajiri watumishi wapya kujaza nafasi hizo.
Mei mwanzoni Rais Magufuli aliagiza hadi Mei 15 mwaka huu watumishi wote waliotajwa katika orodha ya wenye vyeti vya kughushi waondoke mara moja la si hivyo watachukuliwa hatua za kisheria.
SIKILIZA WIMBO MZURI UNAOPINGA ULAWITI KWA WATOTO 
Song: Anza SaSa
Artist: Fresh Andy ft Stino & K-Sam
 
FOLLOW NA LIKE PAGE YANGU YA FACEBOOK HAPA CHINI
 CLICK HAPA OPEN
FOLLOW ACCOUNT YANGU YA INSTAGRAM 
CLICK HAPA ➼ OPEN

MuroTV na murotv.blogspot.com zipo kwaajili ya kukuhabarisha kwa wakati.
Image may contain: text       KWA MATANGAZO WASILIANA NAMI KUPITIA;



Phone: 0768786851
Email:prospermuro690@gmail.com
          : prosperalphonce35@gmail.com
Instagram: muro_tv

No comments:

Powered by Blogger.