Header Ads

BREAKING: TETEMEKO JINGINE LATOKEA KANDA YA ZIWA

BreakingNews

BREAKING: Tetemeko jingine latokea kanda ya ziwa

By Muro Tv
Ni habari za leo May 25 2017 mchana kutokea upande wa kanda ya ziwa ambako bado Wakazi wa eneo hilo hawajasahau tetemeko lililogharimu maisha ya watu na mali zao kwa upande wa Kagera.
Habari ya leo ni kwamba tetemeko limeripotiwa kutokea hukohuko Kanda ya ziwa kwenye maeneo ya Mwanza na Geita lakini hakuna madhara yaliyoripotiwa mpaka sasa.
Japo halijasababisha uharibifu wowote tetemeko hilo la leo ambalo inaripotiwa limechukua kuanzia sekunde 7-10 limesababisha baadhi ya waliokuwemo kwenye majengo ya gorofa  ambayo ni Mwanjonde Block, Administration Block, Academic Block, Library Block (Mario Mgulunde Learning Resource Centre) na Majengo mengine kutoka kwenye majengo hayo wakiwemo Wanafunzi Pamoja na wafanyakazi wa SAUT Mwanza.

MURO TV ilikuwepo mubashara kabisa eneo la tukio, habari nzuri ni kwamba Tetemeko hilo halikuwa kubwa sana kama lile la hivi karibuni na hakuna hata mtu mmoja alieripotiwa kuumia ama kupata mshutuko uliompelekea matatizo.

                  MURO TV Inawapa pole watu wote wa kanda ya ziwa kwa tukio hilo

No comments:

Powered by Blogger.