Kocha wa
Man United Jose Mourinho ambaye usiku wa September 12 2017 aliiongoza
Man United katika mchezo wa
UEFA Champions League dhidi ya
Basel na kufanikiwa kupata ushindi wa magoli 3-0, ameamua kuweka wazi kwa nini hakumtumia
Ander Herrera.
Ander Herrera alicheza game yake ya kwanza ya msimu wa Ligi Kuu
England weekend iliyomalizika
Man United ikiambulia sare ya 2-2 dhidi ya
Stoke City lakini kiungo huyo aliachwa katika mchezo wa jana wa
Champions League dhidi ya
Basel.
Jose Mourinho ameweka wazi kuwa maamuzi yake hayo yalikuwa ya kiufundi wala hakuna sababu nyingine kwa sababu aliamua kutumia viungo wawili
Matic,
Pogba na
Herrera kumuacha.
“Hakuna sababu za ziada kwa Herrera
kuwa nje, game ambayo tuliamua kutumia viungo watatu Herrera alicheza
lakini tulitumia viungo wawili tu Matic na Pogba na walicheza vizuri
hivyo hatukuona sababu ya kufanya mabadiliko, hata
hivyo Fellaini na Carrick walikuwepo benchi pia ” >>> Jose Mourinho
No comments:
Post a Comment