Header Ads

Hii Kali: Siku ya kuzaliwa Rais Mugabe kuwa Siku ya Kitaifa Zimbabwe

Serikali ya Zimbabwe imetangaza kuwa siku ya kuzaliwa Rais Robert Mugabe ambayo ni 21 February itaadhimishwa kama sikukuu ya kitaifa.
Tangazo hilo limetolewa August 18, 2017 na Waziri wa Mambo ya Ndani Dr. Ignatius Chombo akisema hilo ni kwa ajili ya heshima ya Rais Mugabe ambaye ameiongoza Zimbabwe tangu ilipopata Uhuru.
Siku hiyo itaitwa ‘Robert Gabriel Mugabe National Youth Day’.
Mbali na heshima hiyo, Miji na Majiji mengi ya Zimbabwe ina barabara zilizopewa jina lake.

No comments:

Powered by Blogger.