“Walioshindwa kuviendesha Viwanda akiwemo Mbunge wa CCM wavirudishe” – Rais JPM
Rais wa Magufuli
amewaagiza viongozi wa Manispaa ya Morogoro na viongozi wa Mkoa huo
kuwaacha wafanyabiashara wadogo wadogo waendelee kufanya biashara zao
katika eneo la Kituo Kikuu cha mabasi, Msamvu.
Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo July 27, 2017
baada ya msafara wake uliokuwa unatokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam
kusimamishwa na wananchi eneo la Msamvu na kumueleza kero ya kunyanyaswa
na Manispaa wakifukuzwa katika maeneo wanayofanyia biashara hasa baada
kituo cha mabasi cha Msamvu kujengwa upya.
Mbali na hilo, Rais Magufuli amemuagiza
RPC Morogoro SACP – Ulrich Onesphory Matei kuhakikisha Askari Mgambo
hawawasumbui wafanyabiashara wadogo wadogo na kuwataka wafanyabiashara
hao kutofanya vurugu wakati utaratibu mzuri unaandaliwa kwa ajili yao.
Aidha, Rais Magufuli amewataka watu
waliobinafsishiwa viwanda mbalimbali mkoani Morogoro kuvirejesha
Serikalini kama wameshindwa kuviendeleza ili wapewe wawekezaji wengine
wenye uwezo wa kuviendeleza na kuzalisha ajira.
>>>”Ninarudia wito
wangu nilioutoa nyuma, kwamba wenye viwanda hapa Morogoro ambao
wameshindwa kuviendesha, akiwemo Mbunge wa hapa wa CCM ambaye
alibinafsishiwa viwanda vingi, kama ameshindwa kuviendesha avirudishe
ili tuwape watu wengine kwa sababu vijana hawa wanakosa ajira,
nazungumza kwa uwazi kwa sababu msema kweli ni mpenzi wa Mungu.” – Rais Magufuli.
No comments:
Post a Comment