Sababu za Mahakama ya Kisutu kumpa dhamana Tundu Lissu leo
Leo July 27, 2017 ikiwa ni takribani siku 7 tangu Rais wa TLS na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu kukamatwa na kuwekwa mahabusu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imempa dhamana.
Lissu ambaye anatetewa na Mawakili 18, wakiongozwa na Fatma Karume amepata dhamana kwa kutimiza masharti baada ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kutupilia mbali ombi la upande wa mashtaka la kumnyima dhamana.
Katika uamuzi huo, Hakimu Mashauri amesema upande wa mashtaka ulishindwa kutaja kesi ambayo Tundu Lissu aliwahi kuruka dhamana.
Aidha, kuhusu kutopewa dhamana kwa ajili ya usalama wake, Hakimu Mashauri
amesema sababu hiyo haijitoshelezi kumuweka ndani akisema kundi la
Mawakili 18 waliojitokeza kumuwakilisha ni kuonesha upendo wa watu juu
yake hivyo kusimama kidete.
Kutokana na hatua hiyo, Hakimu Mashauri amemuachia kwa dhamana Tundu Lissu
kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika ambao kila mmoja
alisaini bondi ya Tsh. Milioni 10 huku akitakiwa pia kutotoka nje ya Dar
es Salaam bila kibali cha Mahakama.
No comments:
Post a Comment