Maneno 4 Rahisi Lakini Muhimu Ambayo Mke Anahitaji Kusikia Kila Siku
Mawasiliano mazuri kati ya mke na mme ni muhimu sana kwa ajili ya
ustawi wa mahusiano ya wawili wapendanao. Inasemwa kuwa kuvunjika kwa
mawasilioano pekee katika mahusiano kunasababisha mifarakano au
kuvunjika kwa mahusaiano kati ya mke na mme kuliko sababu nyingine.
Wataalamu wa mapenzi na hisia za binadamu wanaeleza kuwa wanawake
wanaguswa sana kwa maneno kuliko vitendo. Sauti na maneno mazuri ni vitu
ambvyo vinawafanya wawe katika wakati mzuri sana kihisia. Wanaume wao
wamefahamika kuwa wanavutwa zaidi kwa kuona kuliko kusikia.
Kwa msingi huu basi ni muhimusana kwa wanaume walio katika mahusiano
ya mapenzi kufahamu siri hii juu ya wenza wao wanawake. Ukitaka kuifanya
siku ya mpenzi wako nzuri basi zingatia maneno yako na sauti yako iwe
katika kiwango kinachofaa.
Yafuatayo ni maneno manne muhimu kuyasema kila siku kwa mkeo na
yataleta mabadiliko makubwa katika mahusiano yenu. Maneno haya
yanalainisha moyo,yanajenga uaminifu,yanazidisha upendo,yanaponya
majeraha ya mapenzi na yanaleta furaha kati ya wapenzi:
Neno #1. “Wewe Ni Mwanamke Mzuri”
Inawezekana uzuri ni sababu mojawapo ya kumuoa au kuwa naye. Basi
hakikisha unamkumbusha kila mara. Wanawake wanahitaji sana kuhakikishiwa
kuwa ni wazuri na wanavutia. Ni hatari sana kama hufanyi hivi kwa
mkeo,nakuhakikishia wanahitaji kusikia maneno haya. Usipomwambia kuna
mtu atamwambia barabarani au kazini na hii ni hatari.
Wanawake wasio ambiwa mara kwa mara kuwa ni wazuri huhangaika sana
juu ya kubadilisha mavazi yao na vipodozi. Ikibidi wanaweza wakafikia
kuvaa mavazi yasiyo na heshima sana kwa mtazamo wa jamii anayoishi. Hii
ni katika kutafuta mrejesho kuwa ni mzuri.
Kama anatumia sana vipodozi na wewe hupendi basi mwambie ni mzuri hasa akiwa asilia,hivyo hahitaji vipodozi vingi.
Neno #2. “Umependeza”
Hili linaendana na la kwanza hapo juu lakini kupendeza sio lazima uwe
mzuri. Uzuri unaweza ukawa wa sura,umbo au tabia zake. Kupendeza ni
kutokana na mapambo na mavazi ambayo mtu anavaa.
Kama kuna mambo makubwa ambayo yanawachukulia muda mwingi wanawake
wengi basi ni urembo hasa wa mavazi,nywele na vipodozi. Wafanya biashara
wajanja wanaweka nguvu zao eneo hili – kutoa huduma za wanawake.
Wanawake wanahitaji sana kuonekana wamependeza hasa toka kwa wapenzi
wao. Mrejesho huu ni muhimu kwao na kunawafanya wajisikie vizuri
,kujiamini na kujiona wa thamani. Mwambie mkeo kila siku asubuhi akitoka
nyumbani au kila mnapotoka pamoja. Mwambie kila akibadilisha aina ya
ususi wa nywele zake.
Neno #3: “Asante”
Kwa kweli mke ndiye mtendaji wa mambo mengi nyumbani. Hata kama kuna
wasaidizi bado kunahitaji uongozi na bila shaka mke ni kiongozi wa yote
haya nyumbani kwa walio wengi.
Utakuta nguo ni safi,chakula ki tayari,watoto wameoshwa na kuvalishwa na mengine mengi. Kuna kila sababu ya kusema “asante”.
Asante ina maajabu makubwa kama ikitolewa kwa jinsi inavyostahili na
kwa dhati. Kwanza humfanya anayeambiwa ajione wa thamani sana kwako.
Pili humfanya anayefanya aongeze bidii kwa yale anayoyafanya.
Hivyo usiache kushukuru kila siku kwa yale mkeo anayoyafanya.
Kunawezekana mengine yakawa si mazuri,lakini hakutakosekana zuri la
kushukuru.
Mwambie “Asante Mpenzi” , “Asante Mke Wangu” na maisha yenu yatakuwa mazuri na yenye furaha.
Fanya kwa vitendo pia,mfano nunua hata kitenge tu na umshangaze kwa
zawadi. Mwambie “asante kwa kuwa mama mzuri wa watoto wetu” au “Asante
kwa kuwa mke mzuri na rafiki mzuri kwangu”.
Neno #4: “Nakupenda”
Kupendwa ni mojawapo ya vitu ambavyo binadamu anahitaji sana.
Chukulia mtoto mfano,toka tukiwa watoto kupendwa ni kitu kinachohitajika
sana na kinapokosekana kuna madhara makubwa yanayotokea ikiwemo mtoto
kutojipenda mwenyewe na kutojiona wa thamani. Kwa wanawake
halikadharika,japo ni wakubwa tayari lakini kasumba ya utotoni imo bado
ndani yetu na mahitaji ni yaleyale.
Ukiangalia vizuri mahangaiko yote ya mwanamke juu ya urembo na mavazi
utaona kuwa ni kutaka kuhakikisha kuwa anapendwa. Au kujinyima na
kuishi katika mwenendo ambao wewe kama mume unafikiri ni vizuri au jamii
inafikiri ni vizuri ni kutaka kuhakikisha kuwa anapendwa. Basi kwa
kumtamkia kuwa unampenda mara nyingi kadili utakavyoweza inampa
kujiamini kwa jinsi alivyo na kwa yale anayoyafanya.
Kumwambia mkeo kuwa unampenda na kuonyesha kwa matendo kunamfanya naye akupende zaidi.
Neno hili likitumika kwa dhati na sio kusema tu lina maajabu makubwa katika kuboresha mahusiano ya wenza wapendanao.
Fanya kwa Dhati na Upendo
Maneno haya manne yana maajabu makubwa kama yakitekelezwa ipasavyo.
Kwanza ni muhimu sana ukayasema kwa dhati na kumaanisha toka moyoni.
Kunaweza kukawa na mambo yasiyofikia viwango vya kushukuru au kusifia
lakini uanaweza ukaanza na yale machache yaliyopo. Baadae utagundua kuwa
hata mengine yanarekebishwa na kufanywa kwa uzuri.
Maajabu ya maneno haya ni katika kubadilisha moyo wa mke na tabia na
matendo yake. Ukiyatumia kwa kiasi kinachofaa na kwa kuyamaanisha
utafanikiwa na utaboresha mahusianao yenu.
Kama una mawazo ya kuchangia mada hii tuandikie katika kisanduku cha majibu hapa chini.
No comments:
Post a Comment