OKWI MAMBO SAFI MSIMBAZI, KUTUA JUMAMOSI KUSAINI MKATABA WA MIAKA MIWILI
Shauku
ya mashabiki wa klabu ya Simba kumwona mchezaji wa zamani wa klabu
hiyo, Emmanuel Okwi kutua kwenye klabu hiyo kwa mara nyingine ni dhahiri
sasa imekaribia kutimia kwa hali ilivyo sasa kati ya uongozi wa Simba
na Okwi.
Hilo
limethibitishwa na Mwenyekiti wa kamati ya Usajili wa Simba, Zacharia
Hans Pope kuweka wazi kuwa tayari klabu imefikia makubaliano na Okwi na
jumamosi ya Juni, 24 ataingia nchini akitokea kwao Uganda kwa ajili ya
kusaini mkataba wa miaka miwili.
“Nimezungumza
nae na tumefanya makubaliano, ataingia hapa jumamosi kusaini mkataba wa
miaka miwili … Okwi ni mchezaji mzuri ambaye amekuwa akitupatia matokeo
mazuri na ni mchezaji ambaye ana uwezo wa kubadilisha matokeo ndani ya
sekunde moja, wote tunafahamu uwezo wake,” alisema Hans Pope.
Aidha
Hans Pope amezungumza kuhusu picha aliyopiga na Okwi na kusambaa kwenye
mitandao na kufanya mashabiki wa soka waamini kuwa tayari amesaini
Simba na kusema kuwa alikuwa Kampala, Uganda kwa shughuli zake binafsi
na ile picha walikuwa wamekutana kufanya mazungumzo
MuroTV na murotv.blogspot.com zipo kwaajili ya kukuhabarisha kwa wakati.
KWA MATANGAZO WASILIANA NAMI KUPITIA;
Phone: 0768786851
Email:prospermuro690@gmail.com
: prosperalphonce35@gmail.com
Instagram: muro_tv
MuroTV na murotv.blogspot.com zipo kwaajili ya kukuhabarisha kwa wakati.
KWA MATANGAZO WASILIANA NAMI KUPITIA;
Phone: 0768786851
Email:prospermuro690@gmail.com
: prosperalphonce35@gmail.com
Instagram: muro_tv
No comments:
Post a Comment