Bomu kubwa la vita vya pili vya dunia kuharibiwa Ujerumani

Watu wakihama
Karibu watu 65,000
wakazi wa mji Frankfurt wamendoka makwao kutoa nafasi kwa wataalamu
wanaoharibu bomu kubwa ambalo lilikosa kulipuka wakati wa vita vya pilia
vya dunia.
Polisi wanasema kuwa shughuli ya kuharibu bomu hilo
ilianza kufuatia kuhamishwa watu wengi zaidi katika historia ya
Ujerumani baada ya vita.Maeneo yaliyohamishwa watu ni pamoja na hospitali, makao ya watu wazee na benki kuu ya Ujerumani

Wenyeji wengi walisema kuwa wangetumia muda wao mwingi siku ya leo kutembelea familia, kuzuru sehemu tofauti za mjii hadi itakapobainika kuwa eneo hilo liko salama.

Helkopta zikipiga doria
Polisi walivyambia vyombo vya habari kuwa shughuliya
kuwahamisha watu ilikuwa imepangwa na kwamba kila mtu alikuwa
ameondolewa eneo hatari.
Wakazi wanaweza kushi kwenye makao ya muda

No comments:
Post a Comment