Waacha kumsaidia aliyezama kwenye maji na kumrekodi kwa simu hadi akafa
Polisi wa Florida wamesema hawatowafungulia mashtaka ya kosa la
mauaji wavulana watano ambao walitumia simu kumrekodi mtu mmoja
aliyekuwa anazama kwenye bwawa la maji hadi kufa bila kumsaidia wala
kutoa taarifa Polisi.
Katika video ya urefu wa zaidi ya dakika mbili, wavulana watano wa
umri wa kati ya miaka 14 na 16 wanasikika wakicheka huku wakimrekodi kwa
simu mtu mmoja aliyekuwa anazama kwenye bwawa jirani na nyumbani kwao
Florida.
Licha ya mtu huyo kuomba msaada, wavulana hao waliendelea kulirekodi
tukio hilo kwa simu huku wakicheka hatua za mwisho wa mhanga huyo
wakisikika wakisema “Anakufa” lakini hawakwenda kutoa msaada wala
hawakutoa taarifa.
Polisi wanasema tukio hilo lilitokea July 9, lakini wavulana hao
licha ya kulirekodi hawakutoa taarifa kwa mamlaka hivyo kuufanya mwili
wa mtu huyo aliyefahamika kwa jina la Jamel Dunn aliyekuwa na umri wa
miaka 31 kukaa kwenye maji kwa zaidi ya siku nne hadi pale familia yake
ilipotoa taarifa za kupotea kwake July 12 na mwili wake ukaopolewa
kwenye maji July 14.
Wavulana hao hawatashtakiwa kwa sababu
Jimbo la Florida kwa sasa halina sheria zinazomlazimisha raia kutoa au
kutotoa msaada kwa yeyote:>>>”Kama ingalikuwepo (sheria ya namna hiyo) tungaliwashtaki.” Msemaji wa Idara ya Polisi ya Cocoa, Yvonne Martinez aliiambia CNN kwa njia ya simu.
No comments:
Post a Comment