TRUMP KUTANGAZA MSIMAMO WAKE KUHUSU MAKUBALIANO YA PARIS
MuroTv
Trump kutangaza msimamo wake kuhusu makubaliano ya Paris
Vyombo vya habari
vya marekani vinasema rais Trump anatarajia kutangaza kujitoa kwenye
makubaliano ya mabadiliko ya tabia nchi yaliyowekwa mjini
Paris,Ufaransa.
Rais Trump mwenyewe aliandika katika ukurasa wake wa Twitter kuwa anatoa tangazo hilo hivi karibuni.
Kujitoa katika harakati hizo za mabadiliko ya tabia nchi ni miongoni mwa vipaumbele ambavyo alivitaja wakati wa kampeni zake za urais ingawa hivi karibuni rais huyo alikaririwa kusema kuwa bado hajafanya maamuzi.
Mkutano wa nchi zenye uchumi mkubwa G7 uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita ,uliolenga kupunguza shughuli zinazongeza uzalishaji wa hewa chafu ili kupuguza athari za mabadiliko ya tabia nchi kama ilivyokubaliana na nchi takribani mia mbili jambo ambalo rais Trump alikuwa hajaliridhia.
- Trump 'atengwa' na wenzake G7
- Mataifa ya G7 yakataa kuiwekea Urusi vikwazo
- Viongozi wa G7 waangazia bara la Afrika
No comments:
Post a Comment